Monday, June 30, 2014
Mzee wa kanisa Aumbuka baada ya kufumaniwa Gesti na kibinti kidogo kilicho chini ya miaka 18
Mzee wa kanisa la kiroho (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyetajwa kwa
jina la Luca Pesa, mkazi wa Segerea, Dar, ameaibika baada ya kukurupushwa
kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) akidaiwa kutaka kuvunja amri ya sita na
binti ambaye ni msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Debora Jacob.
Tukio hilo ambalo kamwe Luca hawezi kulisahahu maishani mwake,
lilijiri kwenye gesti hiyo iliyopo karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha
Segerea, Dar, Jumanne iliyopita huku mzee huyo akishushiwa tuhuma nzito ya
rushwa ya ngono kwa vibinti chini ya miaka 18.
Katika tukio hilo, mzee huyo wa kanisa na msanii huyo wa Kundi la
Maigizo la Vivif lenye maskani yake maeneo hayo walikuwa wamejichimbia kwenye
gesti hiyo katika chumba ambacho mlangoni kilikuwa kimeandikwa Rombo kabla ya
kuchomolewa na kufikishwa kanisani kisha polisi.
Fumanizi hilo lilikuwa limesukwa
na wasanii wa
kundi hilo kwa
lengo la kumkomoa
mzee huyo wa
kanisa ambaye alikuwa
ni mfadhili wa kundi lao
aliyeanza kutumia mgongo
wa ufadhili kuwatongoza
mabinti wa kundi
hilo mmoja baada
ya mwingine.
Wakiwa ndani ya gesti
hiyo, wasanii wa kundi
hilo walivamia chumba
hicho na kuanza
kumchomoa mzee huyo
ambaye aliruka ukuta na
kudondokea kwenye matuta ya viazi.
Akiwa anajizoazoa kwenye matuta hayo, kundi la wasanii hao
lilimuunganishia ambapo kabla ya kumnasa aliingia kwenye chumba cha nyumba
iliyopo jirani na gesti hiyo ili kujisalimisha.
Hata hivyo, zoezi lake lilifeli baada ya wasanii hao kumtahadhalisha
mwenye nyumba hiyo kuwa wanamtaka mtuhumiwa wao la sivyo wangeichoma moto.
Baada ya kuzingirwa na wasanii hao huku akihatarisha maisha yake kwa
kuwa wasanii hao walikuwa na hasira, aliona yasiwe makuu akaamua kuwaruhusu
wamtoe mtuhumiwa wao wakamalizane naye kanisani.
Alipotiwa mikononi, mzee huyo wa kanisa aliomba apelekwe kanisani
ambapo hapakuwa mbali na eneo la tukio ili akahifadhi vitu vyake muhimu pamoja
na kuomba ushauri.
Kundi hilo la wasanii lilimpeleka kanisani msobemsobe ambapo baada ya
hatua kadhaa polisi walitokea na kuwadhibiti wananchi wenye hasira na wasanii
waliotaka kumdhuru mzee huyo wa kanisa wakati akipelekwa kanisani.
Wakiwa mitaani, njiani mabinti walikuwa wakipiga kelele
‘weraaa…ukomeee…’ huku wakifurahia kufunga mitaa kwa madai kwamba mzee huyo wa
kanisa alizidi.
Katika sekeseke hilo, polisi hao walimtia pingu mzee huyo wa kanisa na
kuongoza safari ya kuelekea kanisani.
Wakiwa kanisani hapo polisi walijitambulisha na kuwauliza wachungaji
pamoja na waumini wa kanisa hilo kama walimfahamu mzee huyo wa kanisa.
Kundi la wazee pamoja na vijana wa kanisa hilo walikiri kuwa Luca ni
mmoja wa wazee wa kanisa hilo ndipo polisi hao wakamruhusu kuwakabidhi baadhi
ya vitu vyake ikiwemo simu na fedha kisha breki ya kwanza ikawa Kituo cha
Polisi cha Tabata-Shule ambapo alifunguliwa jalada la kesi namba;
RB/3843/2014
-RUSHWA YA NGONO, KUWAWEKA KAMBI KINYUME CHA SHERIA WASICHANA WENYE UMRI CHINI
YA MIAKA 18 NA KUWADHALILISHA KIJINSIA.
Mungu hashindwi: Hatimaye Flora Mbasha na mumewe wapatana....... Mwanasheria asimamia kila kitu, vigogo nao waingilia kati sakata hilo
Hakuna neno zuri la
kusema zaidi ya Mungu mkubwa. Ule mtafaruku ndani ya ndoa ya mwimba Injili
mahiri Bongo, Flora na mumewe, Emmanuel Mbasha umedaiwa kumalizika kwa wawili
hao kupatana.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, wawili hao walikalishwa kikao
cha upatanishi mapema wiki hii kilichokuwa chini ya familia.
MANENO YA CHANZO
“Kikao cha familia kilikaa, Mbasha aliitwa akafika, Flora naye
aliitwa akatokea, mazungumzo yalikuwa marefu lakini kimsingi waliamua kuweka
kando mtafaruku wao na kuijenga upya ndoa yao,” kilisema chanzo.
Chanzo kiliongeza kuwa katika kikao hicho cha mwanzoni mwa wiki
hii, miongoni mwa adidu za rejea ilikuwa kutokumbushia vikao vilivyopita ambapo
hakukupatikana muafaka.
VIKAO VILIVYOPITA
Katika vikao vilivyopita, wahusika wakuu walikuwa wazazi wa
Mbasha (mzee Maneno Mbasha, Zulfa Maneno), ndugu wa Flora na Mchungaji wa
Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
VIKAO VYA BAADAYE
Kwa mujibu wa chanzo, vikao vilivyofuata, wawili hao wakawa
tayari kila mmoja ametema nyongo yake pembeni na kufikia makubaliano kwamba,
ndoa yao isimame tena wakitumia maandiko kwenye Biblia kutoka kitabu cha
Waebrania yanayosema: Ndoa na
iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi
Mungu atawahukumia adhabu.
WAKORINTHO YAFUNGA KAZI
Kwa mujibu wa chanzo hicho, maneno mengine ya Biblia
yaliyotumika kwenye kikao hicho mpaka wawili hao wakaamua kurudiana ni 1
Wakorintho 7:1-10 ambapo maandiko yanasema:
Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake
mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki
yake vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
Mke hana amri juu ya mwili wake bali mumewe vivyo hivyo mume
hana amri juu ya mwili wake bali mkewe. Msinyimane, isipokuwa mmepatana kwa
muda ili mpate faragha kwa kusali, mkajiane tena shetani asije akawajaribu kwa
kutokuwa na kiasi kwenu.
Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza, wala hapo si mimi, ila
Bwana (Mungu), mke asiachane na mumewe, lakini ikiwa ameachana naye na akae
asiolewe au apatane na mumewe, tena mume asimwache mkewe.
KIKAO CHA JUMAMOSI KUMALIZIA
Chanzo kilisema kuwa, kikao cha mwisho ambacho kitamalizia
kuweka mambo sawa ili wawili hao waanze ngwe ya pili ya ndoa yao ambayo
inaaminika itakuwa ya mwisho mpaka kifo kiwatenganishe, kinatarajiwa kufanyika
leo jijini Dar es Salaam mahali ambapo hapakutajwa.
MWANASHERIA ATAJWA
Mwanasheria wa Flora aliyejulikana kwa jina moja la Ado ametajwa
kusimamia kikao hicho ili wawili hao waanze maisha mapya baada ya safari fupi
ya mvurugano uliowafanya kuwa mbalimbali.
Juzi, Risasi Jumamosi lilimsaka mwanasheria huyo kwa njia ya
simu yake ya mkononi ili kumsikia anasemaje kuhusu kutajwa kwenye usuluhishi wa
ndoa hiyo ambapo alipopatikana alisema:
“Niko Arusha, Ijumaa nitarudi Dar. Kuhusu kikao cha usuluhishi
siwezi kukwambia lakini suala la kuwapatanisha nalifahamu, nawaomba na ninyi
msaidie kufanikisha jambo hilo zuri.”
VIPI KUHUSU KESI YA MADAI YA KUBAKA?
Hata hivyo, Wakili Ado hakutaka kugusia kuhusu kesi ya Mbasha
iliyopo Mahakama ya Wilaya ya Ilala ambapo anadaiwa kumbaka shemejiye mara
mbili (jina tunalo) ambayo kwa mujibu wa mahakama, upelelezi umekamilika na
itasikilizwa Julai 17, mwaka huu.
KWA UPANDE WAKE FLORA
Risasi Jumamosi lilimwendea hewani, Flora ili kumsikia anasemaje
kuhusu kuwepo kwa upatanishi kati yake na mumewe, Emmanuel.
Huyu hapa: “Ongea na wakili wangu atakwambia kila kitu.” Ambapo
majibu ya wakili yalikuwa: ”Ninachojua mimi ni kwamba Flora ameshamsamehe
mumewe na yuko tayari kuanza ukurasa mpya.”
MBASHA SASA
Kwa upande wake, Mbasha alipozungumza na Risasi juzi alisema
kurejea upya kwa ndoa yake ni jambo la kuupendeza moyo wake.
“Mimi sina neno nipo tayari, nimeshasamehe yaliyotokea, Flora ni
mke wangu jamani, nampenda sana kutoka moyoni.”
Chanzo: Risasi jumamosi
/Gpl
DAVIDO WINS BEST INTERNATIONAL ACT AFRICA AT THE 2014 BET AWARDS
Weeks after “ruling”
the 2014 MTV Africa Music Awards with multiple awards, Nigerian music star,
Davido has again won the Best International Act – Africa award at the 2014 BET
Awards 2014, which held last night at the Nokia Theater, Los Angeles, USA.
Davido beat
Mafikizolo, Tiwa Savage, Sarkodie, Toofan and Diamond Platnumz for the win.
The entertainer
broke the news on his Instagram page with the photo and a caption which read:
“Thanks to my fans!!! WE WON! BET BEST AFRICAN ACT 2014!! Time to party!!!”
ALICHOKISEMA DIAMOND BAADA YA TUZO YA BET ALIYOKUWA AKIWANIA KUCHUKULIWA NA DAVIDO WA NIGERIA
"Tusipopenda kukubali matokeo na ushindi wa wenzetu basi daima hatutaweza kuwa washindani, muhimu ni kujua wapi tulipotoka na wapi tulipo leo.
"Katika nchi zaidi ya 20 zenye wasanii zaidi ya milioni 40 kuchaguliwa Tanzania ni fursa, heshima na hatua kubwa.
"Cha muhimu ni kuitumia vyema fursa hii na kuhakikisha mwakani tunapiga hatua, asante sana kwa wote wanaozidi kunisupport"
Sunday, June 29, 2014
WHO URGES 'DRASTIC ACTION' ON EBOLA, CALLS 11-NATION MEETING
![]() |
WHO calls for 'drastic action'
to fight the deadliest Ebola outbreak on record, as it announces an 11-nation
meeting to address the growing crisis.
|
GENEVA - The World Health Organization on Thursday called for "drastic
action" to fight the deadliest Ebola outbreak on record, as it announced
an 11-nation meeting to address the growing crisis.
As of Sunday, 635 cases of haemorrhagic fever (most confirmed to be Ebola),
including 399 deaths, have been reported across Guinea, Liberia and Sierra
Leone, making the outbreak the largest ever "in terms of the number of
cases and deaths as well as geographical spread," WHO said.
"Drastic action is needed," the UN agency stressed in a
statement, warning of the danger that the virus could jump to other countries.
Earlier this week, medical charity Doctors Without Borders (MSF) also said
the outbreak of the virus, which is deadly in up to 90 percent of cases, was
"out of control".
Since west Africa's first-ever epidemic of the deadly haemorrhagic fever
emerged in Guinea in March, WHO has sent in more than 150 experts to help
tackle the crisis.
Despite the efforts of the WHO and others, there has been a
"significant increase" in the number of cases and deaths reported
each day for the past three weeks, it said.
The agency is now "gravely concerned (by) the on-going cross-border
transmission into neighbouring countries as well as the potential for further
international spread," said WHO's regional director for Africa, Dr. Luis
Sambo.
"This is no longer a country specific outbreak but a sub-regional
crisis that requires firm action by governments and partners," Sambo
warned.
WHO's top Ebola specialist Pierre Formenty told AFP last week the recent
surge in cases had come in part because efforts to contain the virus had been
relaxed too quickly after the outbreak appeared to slow down in April.
"One case can restart an entire epidemic," he warned, justifying
the dramatic measures needed to contain the virus, which spreads through bodily
fluids including sweat, meaning you can get sick from simply touching an
infected person.
To address the growing crisis, the WHO said Thursday it would convene a
meeting of the health ministers from 11 countries in Accra, Ghana on July 2 and
3 "to discuss the best way of tackling the crisis collectively as well as
develop a comprehensive inter-country operational response plan."
Ministers from Guinea -- where nearly 400 confirmed, suspected and probable
cases have surfaced so far, including 280 deaths -- and Liberia, which counts
63 cases and 41 deaths, will take part in the meeting.
Sierra Leone, which has seen 46 confirmed Ebola deaths, will also be there.
In addition, neighbouring countries Ivory Coast, Mali, Senegal, Guinea
Bissau and Gambia, along with Ghana, and countries as far afield as Uganda and
the Democratic Republic of Congo, where Ebola was first detected nearly 40
years ago, have also been invited, WHO said.
A range of UN agencies and other aid organisations including MSF and the
Red Cross, as well as the western African, US, British and EU centres for
disease control, WHO said.
WHO has described the current epidemic as one of the most challenging since
the virus was first identified in 1976 in what is now the Democratic Republic
of Congo.
That outbreak, until now the deadliest, killed 280 people, according to WHO
figures.
Ebola is a tropical virus that can fell its victims within days, causing
severe fever and muscle pain, weakness, vomiting and diarrhoea -- in some cases
shutting down organs and causing unstoppable bleeding.
No medicine or vaccine exists for Ebola, which is named after a small river
in the DRC.
DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE GOES LIVE USING SA COMPANY’S TECHNOLOGY
The Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) went live using South
African software company Securities and Trading Technology’s (STT) trading and
settlement technology on Friday morning.
STT was chosen in April to provide the
Tanzania exchange with solutions to improve its trading ability and the plan is
to increase the number of securities and bonds traded in Tanzania from the
current 25 companies.
CEO of the Dar es Salaam Stock Exchange
Moremi Marwa said on Friday the new system would help them achieve “true
delivery” and improve risk management for investors.
“This is in line with our strategic
intent of introducing new products and increasing accessibility to our system
through the use of mobile‚ internet and SMS trading facilities‚” he said.
MD of STT Michelle Janke said the
Tanzanian exchange had become her company’s third exchange to go live using its
integrated exchange solution.
Further‚ Tanzania is the company’s
first African exchange to go live with its equities platform‚ as well as its
Central Securities Depository system.
Thursday, June 26, 2014
AFRICA TO HOST APRM MEET IN DAR
The
21st meeting of the Heads of State and Government participating in the African
Peer Review Mechanism (APRM) has decided to conduct Continental wide
sensitization seminars and cited Dar es Salaam as one of the venues.
The
news was announced during the APRM meeting held on 24th June 2014, in Malabo -
Equatorial Guinea. The main theme of this year's meeting is 'Promoting Good
Governance for the Well Being of the People of Africa.'
According
to the APRM Tanzania Executive Secretary, Rehema Twalib who is attending the
meetings in Malabo, Tanzania will host a sub-regional level APRM meeting later
this year.
“In
an effort to step up awareness on the APRM process, the Panel has embarked on
regional sensitization workshops. Tanzania has been designated to hold the East
African Workshop which will include participants from all Eastern African
countries,” she said.
A
total of 35 out of 54 AU countries are participating in the APRM process. In
her opening speech, the APRM Chairperson, Madam Ellen Johnson-Sirleaf addressed
issues of sustainability of the APRM process, focusing on a well-coordinated
restructuring of the APRM Continental Secretariat.
The
participating Heads of States reiterated their commitment to fast track the
process. In this regard, four countries including Kenya, Ghana, Nigeria and
South Africa have been lined up for a second Peer Review under the APRM
auspices and countries that are ready of their first Peer Review include; Chad,
Mauritania, Senegal and Liberia.
Tanzania
is a member of the APRM since 2004 and has completed all the initial stages of
the governance review. A Programme of Action is now in place and the government
is working on the identified governance challenges.
ROSE MUHANDO KUZINDUA ALBAMU YAKE YA FACEBOOK AGOSTI 3/2014 JIJINI DAR
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari
kwenye viwanja vya Karimjee leo wakati alipokua akitangaza Uzinduzi mkubwa wa
Albam ya Shikilia Pindo maarufu kama FACEBOOK ya mwimbaji wa muziki wa injili
anayevuma, Rose Muhando utakaofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 3
/2014 jijini Dar es salaam, ambapo amesema baadhi ya mapato yatakwenda
kuviwezesha mitaji zaidi ya vituo 10 vya watoto yatima jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw.
Alex Msama akifafanua zaidi kwa
Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi huo unaoatarajiwa kuwa mkubwa katika ukanda
wa Afrika Mashariki kwa waimbaji wa muziki wa injili.
Subscribe to:
Posts (Atom)